• Call us: +255 222 666 725
  • Email: redeso-hq@redeso.or.tz
Relief to Development Society (REDESO)
SUPPORT US
  • Home
  • About Us
    • Overview
    • Vision and Mission
    • Policies and Procedures
    • Organization Structure
    • Our Partners
    • Our Team
  • Programmes
    • Child Protection
    • Education Equity and Quality
    • Health and Social Protection
    • Livelihood And Community Development
    • Natural Resources, Environment Management And Energy Solutions
  • Branches
  • News & Resources
    • News and Events
    • Reports and Publications
    • Newsletters
    • Photo Gallery
    • Video Gallery
  • Contact Us

Serikali na Wadau Waja na Elimu Juu ya Corona kwa Watoto

  /   News and Resources   /   Serikali na Wadau Waja na Elimu Juu ya Corona kwa Watoto
Apr 08, 2020
Serikali na Wadau Waja na Elimu Juu ya Corona kwa Watoto
08Apr

Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto (Idara Kuu ya Maendeleo ya Jamii) kwa kushirikiana na Mtandao wa Malezi, Makuzi na Maendeleo ya Watoto Wadogo Tanzania (TECDEN), Taasisi ya Chakula na Lishe, Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Watoto (UNICEF) wameandaa mkakati wa kufikisha ujumbe kwa watoto kuhusu kujikinga na maambukizi ya Virusi vya Corona.

Akizungumza leo katika kikao kazi kilichowakutanisha wadau hao jijini Dar es Salaam Mkurugenzi Mtendaji wa Mtandao wa Malezi, Makuzi na Maendeleo ya Watoto Wadogo Tanzania (TECDEN) Bruno Ghumpi amesema kumekuwepo na ujumbe mbalimbali katika kujikinga na maambukizi ya Virusi vya Corona ila kumekosekana ujumbe maalum unaolenga makundi maaalum ikiwemo wanawake wajawazito na watoto wadogo kuanzia miaka 0 hadi minane.

Ameongeza kuwa kuwepo kwa elimu sahihi kwa watoto hao kuhusu ugonjwa wa COVID 19 itawasaidia wazazi au walezi na watoto wenyewe kupata taarifa zitakaziwasaidia kujikinga na Virusi hivyo ili kupunguza au kuondokana na maambukizi ya Virusi hivyo katika maeneo yao.

“Ujumbe huu kwa watoto ni muhimu sana kwani kundi hili kwa sasa lipo nyumbani kutokana na kufungwa kwa shule hivyo ni vizuri wazazi na walezi wakazingatia masuala muhimu ya kuwafundisha watoto wao kujikinga na maambukizi ya virusi vya Corona” amesema

Kwa upande wake Afisa Maendeleo ya Jamii Mkuu kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Idara Kuu ya Maendeleo ya Jamii Bw. Mathias Haule amesema kuwa ni muhimu kwa wadau kuhakikisha wanafikisha elimu katika ngazi ya chini kuanzia familia, kijiji/mtaa ili kuwezesha watu hao kupata taarifa na elimu sahihi juu ya kujikinga na maambukizi ya virusi vya Corona.

“Elimu ifike katika ngazi ya familia hasa katika maeneo ya vijijini ambako bado elimu haijawafikia kwa kasi inayotakiwa ili kuondokana na maambukizi ya virusi vya Corona nchini.” Amesema

Categories

  • News and Events11
  • Conferences0
  • Reports and Publications5
  • Success Stories0
  • Vacancies and Tenders0
  • Newsletters2

Other Posts

  • Apr 24, 25 Financial Statements for the Year Ending 31st December 2023
  • Mar 27, 25 Zaidi ya Vijana na Wanawake 3,000 Kunufaika na Mafunzo ya Nishati Safi
  • Nov 06, 24 REDESO na Mkakati wa Matumizi ya Nishati Safi na Salama Tanzania
  • May 22, 23 Turkish Embassy providing a basket charity for solidarity to Urban Refugees in Dar es salaam.
  • Dec 11, 20 Financial Regulations and Manual

Facebook

Relief to Development Society (REDESO)

Our Address

  • 14110 Kinondoni Mjini, Mtaa wa Urambo, Dar es Salaam, Tanzania
  • redeso-hq@redeso.or.tz
  • +255 222 666 725
  • +255 717 037 311

Quick Links

  • About Us
  • Programmes
  • Our Team
  • Our Members
  • Our Partners
  • News & Events
  • Publications
  • Photo Gallery
  • Video Gallery
  • Contact Us
  • Our Locations
  • Privacy Policy

Follow Us

+255 717 037 311

By subscribing to our mailing list you will get the latest news from us.

SUPPORT US NOW

Whats New

  • Financial Statements for the Year Ending 31st December 2023
  • Zaidi ya Vijana na Wanawake 3,000 Kunufaika na Mafunzo ya Nishati Safi
  • REDESO na Mkakati wa Matumizi ya Nishati Safi na Salama Tanzania
  • Turkish Embassy providing a basket charity for solidarity to Urban Refugees in Dar es salaam.
  • Financial Regulations and Manual
Copyright © 2025 - Relief to Development Society (REDESO)